Nguvu Ya Msamaha Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2014
Lyrics
Nguvu Ya Msamaha - Ambwene Mwasongwe
...
Alisikia minong'ono mtaani
Watu walikuwa wakiteta kuhusu yeye
Masikini huyu hakujijua
Alijiondokea akitikisa kichwa chake
Ahsante sana Bwana umenisaidia
Mabaya hayakunikuta mimi
Kumbe maneno yale yalikuwa yake
Ila bahati mbaya hakuyajua
Alipoyasikia alidhani mapya
Kumbe yalikuwa yanakwisha
Alipogundua Yanamuhusu
Alihangaika ajitetee
Aliwalaumu sana rafiki zake
Kwa kujua wamenyamaza
(Jamani Jamani)
Nyamaza usilie
Mungu atakusaidia
Hajawahi mtupa mtu
Nawe hatakutupa
**
**
Yakamshinda kuvumilia
Mabaya yale
Kila alipowaona wabaya wake
Moyo wake ulipasuka
Akapanda gari
Asijue aendako
Njia nzima alikuwa akiwaza
Kwa nini baba yangu
Amchukue Mke wangu!?
Aliwalilia Watoto wake
Ninawaacha mkiwa wadogo
Sikutamani muishi hivyo
Ila mama yenu kasababisha
Ninakwenda nikafie mbali
Ninasikitika hamtaniona
Nisameheni wanangu
Sitaki babu yenu na Mama yenu
Waone maiti yangu
Mwanangu!!!
Sikia,
Unadhani uchungu
Ulionao moyoni
Unaweza kuondoa
Kwa kuutoa uhai wako!?
Unadhani utaridhika
Kwa kuutoa uhai wako!?
(Je pia Mwanangu )
Je, pia unadhani
Ubaya huu uliotendewa
Unaweza kufutika
Kwa kulipa kiasi!?
**
**
Malaika wa Bwana
Walimfuata alikokwenda
Kila alipojaribu kujiua
Mara zote Hilo lilishindwa
Sauti ya Bwana
Ikasikika ikimuita
Rudi nyumbani
ukawaombe msamaha
Baba yako na Mke wako
Usiende kuwaambia Watoto wako
Ubaya wa mama Yao uliotendewa
Usijemlaumu baba yako
Mbele ya macho yao
Wakasikia
Mimi nakutuma Ninakusudi
Ukifika ukawaangukie
Nataka nijitukuze
Kwa nguvu ya msamaha
Nenda nipo nawe
Usiogope!
Nyamaza usilie
Mungu atakusaidia
(kwa hili nalo)
Hajawahi mtupa mtu
Nawe hatakutupa
(Kwa hili nalo)
Nawe hatakutupa
*
Unajua Mungu unanionea
Wamenikosea Hawakuniomba msamaha
Nilipo ondoka waliniona
Japo watoto wangu na Mama yangu
Sikuwaaga
Iweje leo uniambie nirudi nikawaombe
Wao msamaha Tena!?
Wakati wenyewe
Walipaswa kuniomba msamaha!
*
Ninajua moyo wako
Ulivyoumizwa mwanangu
Ndio maana nakutuma
Upone
Ninakutuma
Nenda kawaonyeshe
Nguvu ya
M---S---A---M---A---H---A