Nyamaza Lyrics
- Genre:R&B
- Year of Release:2021
Lyrics
Nyamaza - Mrkiddo
...
...
weka pombe singara chini
subiri tuongeee
zima kijiti marijuana za nini
ngoja tuongee
mbona ulisema mengi
ukitaka nipoteee
saa umefanya nini na ulisema nini wala usijitetee
macho hayana pazia nilimuona anavutia
nae kanikubalia kumbe moyoni unaumia
Dunia imejaa visanga
ubinadamu umekua majanga
Tembo anaefugwa kwa banda anataka kula kuku pia na vifaranga
Mungu tu akusamehe wewe ni kama ndugu
Upunguze munkalii uadui wa nini mwenzangu eee
ukitenda kosa na hujaomba radhi unakosea(koseea)
Mama yake mzazi huruma ungemuone(oneea)
Chunga kinywa kiwe na kituo hekima ndo iwe funguo
maneno ya nini unajivua nguo
kumbuka ulimwengu ni kama chuo
ungenyamaaza
(kaa kimya)
bora ungenyamaza
(kama huna la maana)
ungenyamaaza
(ukikosa heshima)
bora ungenyamaza
(bora kukaaa kimya)
ungenyamaaza(usiongee)
bora ungenyamaza
(bora ungenyamaza)
ungenyamaza tu
bora ungenyamaza
kua muungwana
......
mmmmh mmh mmh mh
hasira hasara
mimi ni ndungu yako
ukanitoa kafara
ukakesha hukutaka kulala
ukipambana niaribikiwe
kaka wa mtwara
ukasahau mapenzi ni Siri
Tena Siri ya wawili
kilichokuponza maadili tamaa ukashindwa isitiri
Tunza heshima yako na mashabiki zako hadi mbungeni
na unapotongoza warembo boxer usiweke pembenii
macho hayana pazia
nilimuona anavutia nae kanikubalia
kumbe moyoni unaumia
ukitenda kosa na hujaomba radhi unakosea
Mama yake mzazi huruma ungemuonea
Chunga kinywa kiwe na kituo
hekima ndo iwe funguo
Maneno ya nini unajivua nguo
kumbuka ulimwengu ni kama chuo
ungenyamaaza(kaa kimya)
bora ungenyamaza
(kama huna la maana)
ungenyamaaza(ukikosa heshima)
bora ungenyamaza
(bora kukaaa kimya)
ungenyamaaza(usiongee)
bora ungenyamaaza
(bora ungenyamaza)
bora ungenyamaaza tu
bora ungenyamaza
(kuwa muungwana)
....
...
....