Umebadilika ft. Banana Zorro Lyrics
- Genre:Hip Hop & Rap
- Year of Release:2017
Lyrics
Umebadilika ft. Banana Zorro - Msodoki Young Killer
...
lamurete mi vida mikurasoo
teamo teamo miamor
lamurete mi vida mikurasoo
teamo teamo miamor
pokea busu shavuni kutoka kwa mnyamwezi
ambaye uliona nakurubuni mdanganyifu wa mapenzi
leo umeniona kanuni bila mimi jibu uwezi
chozi mwanzo wa uzuni maji huleta utelezi
sasa unalala salama unakumbata picha yangu
usiku njizi inakwama bila sauti yangu
leo zamu yako mama si unakumbuka hasi zangu
kipindi unanitukana unadai sio type yangu
sasa unaniita mchumba unaamini nitakuoa
hadi macho unanifumba hata tongo tongo sijatoa
unanipa hadi mavumba nisifurie nikaboa
unamshukuru muumba zawadi ka mimi kunitoa
si ulinisema kwa baba ako ni kamaa ataniazibu
ukiwa na wenzako mkiniponda kwa zabibu
hukujua nitakuwa wako nitashinda majaribu
ingawa mwaka mzima nilihaso kufuata ili unipe jibu
ni niniiinii kilicho badilika
ni niiiniih kilicho kubadilisha
ama ni miiimiiih nime badilika
siamini mi umekamatika umeshikika
umebadilika weeeeh
ya nini utumbo uutupe ukanipa nikaulia ndizi
mpaka pande za fukwe tukasepa kubalizi
hauna shauku pale unapoona machizi
eti unampenda Belle na Ice ndo wapo easy
unanipa ushauri pamoja tunaujadili
ukasema una nafsi moja huwezi kutupenda wawili
nafasi niliyonayo kwako zaidi ya kunipa nwili
sa ni ndoa hitaji lako umechoka kusubili
sasa haulali hadi unipigie phone
unadai nina kosa kubwa la kuutesa moyo wako
naheshimu hisia zako unavyosema unaniamini
hata vocha ya laki moja haitoshi kuongea na mimi
mapenzi yangekuwa ni maji nahisi ungenioa bahari
mapenzi yangekuwa kipaji nahisi ungenipa mistari
hauutaji ushauliwe juu yangu mwamuzi wewe
unasema moyo wako wangu na mi ndo chaguo la wewe
ni niniiinii kilicho badilika
ni niiiniih kilicho kubadilisha
ama ni miiimiiih nime badilika
siamini mi umekamatika umeshikika
umebadilika weeeeh
nimekupa nini unadai
tofauti na sauti nzuri nayokuimbia kitandani daily unafurahi
ama ni swaga za majinzi na tai
ama ni penzi zuri nalokupa asubuhi kabla ya chai
umechoka kuniita killer unataka uniite mume
mapenzi yangekuwa ajira ungeniajiri kidume
nishakuteka fikira so inabidi tu ujitume
kuniweka sawa kisha tuwazibiti paka shume
unasema ungejua mapema hata usingelinga
ungenipokea kwa kwa moyo mmoja na mikono ungekinga
kwa kiss za kutosha ungeni hug kila saa
na kama ungekuwa malkia ungenihonga hata Dar
sikufichi mamaa unanipa raha
umeshinda vita yako ya mapenzi na sitojiita shujaa
sitaji nishauliwe juu yako mwamuzi mimi
nasema moyo wangu wako na wewe ndo chaguo la mimi
ni niniiinii kilicho badilika
ni niiiniih kilicho kubadilisha
ama ni miiimiiih nime badilika
siamini mi umekamatika umeshikika
umebadilika weeeeh
mmh mmmh
ama nyimbo za mapenzi zimeee kubadilisha
Maneno yangu ya mahaba mpaka umebadilika
siamini mii umebadilika umeshikikaa umekamatika
weeei yeii
Man water
MD classic Msodoki